Coastal Union imepoteza mechi ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Yanga baada ya washabiki wake kuwa chanzo cha Mwamuzi kuvunja mchezo huo uliofanyika Aprili 24, 2016 kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
Uamuzi huo umefanywa na Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana leo (Aprili 27, 2016) jijini Dar es Salaam kwa kuzingatia Kanuni ya 28(2) ya Kombe la Shirikisho. Wakati mechi hiyo inavunjwa, Yanga ilikuwa ikiongoza kwa mabao 2-1.
Pia Coastal Union imepigwa faini ya sh. 2,000,000 (milioni mbili) kwa kuzingatia Kanuni ya 42(26) ya Ligi Kuu kutokana na vitendo vya vurugu za washabiki wake wakati wa mechi hiyo. Pia TFF haitasita kufungiwa uwanja huo iwapo vitendo hivyo vya vurugu za washabiki havitakoma.
Mwamuzi wa mchezo huo Abdallah Kambuzi amefungiwa mwaka mmoja wakati Mwamuzi Msaidizi namba mbili Charles Simon ameondolewa kwenye ratiba ya waamuzi. Adhabu hizo zimetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 38(1) ya Ligi Kuu.
Mchezaji Adeyum Ahmed wa Coastal Union anapelekwa Kamati ya Nidhamu ya TFF kwa ajili ya hatua zaidi kutokana na kitendo chake cha kumpiga kichwa Mwamuzi wa Akiba baada ya kutolewa nje. Hata hivyo, Ahmed hakufanikiwa kutimiza azma hiyo baada ya Mwamuzi huyo kumkwepa.
Yanga imepigwa faini ya sh. 500,000 (laki tano) kwa mujibu wa Kanuni ya 14(13) ya Ligi Kuu kutokana na kutoingia vyumbani kwenye mechi hiyo ya Kombe la Shirikisho.
Vilevile malalamiko ya Coastal Union kutaka mechi hiyo irudiwe yametupwa baada ya Kamati ya Mashindano kubaini kuwa hayana msingi wowote.
Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com
Wednesday, April 27, 2016
Yanga Yatinga Fainali Kombe La Shirikisho
Related Posts:
First Eleven Ya Yanga Hii Hapa Leo Dhidi Ya Al Ahly KIKOSI CHA YANGA KINACHOANZA DHIDI YA AL AHLY LEO, HIKI HAPA… 1. Ally Mustapha 2. Juma Abdul 3. Mwinyi Haji 4. Kelvin Yondani 5. Vicent Bossou 6. Thabani Kamusoko 7. Deus Kaseke 8. Salum Telela 9. Amissi Tambwe 10. Donald N… Read More
"Nisipompanga Cannavaro, Basi Nitampanga Mwingine Mwenye Uwezo" Kauli Ya Hans Kocha wa Yanga, Hans van Der Pluijm amesema nahodha na beki wake wa kati wa timu yake, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ yupo fiti kucheza mechi ya leo dhidi ya Al Ahly ila ni siri yake kuhusu kucheza. Cannavaro ni kati ya wachezaji… Read More
Yanga Na Azam Kuipa TFF Mamilioni Ya Pesa Achana na klabu zenyewe kuneemeka, Azam FC na Yanga zikifuzu kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho basi Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) litapata fedha kutokana ushiriki wa timu hizo. Yanga ipo katika Ligi ya M… Read More
Mgomo Wa Yanga Dhidi Ya Al Ahly Kuelekea Mechi Yao Leo Manji Rais Wa Yanga Uongozi wa Dar Young Africans umegoma kuwauzia wapinzani wao, Al Ahly ya Misri haki za kurusha matangazo ya mechi baina yao Mechi itakayochezwa Leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Yanga ndo wenyeji wa m… Read More
Ndanda Kosovo Afariki Dunia Ndanda Kosovo Enzi Za Uhai Wake Mwananamuziki maarufu wa dansi nchini, Ndanda Kosovo amefariki dunia usiku wa kuamkia leo. Taarifa zinazotufikia, zinaeleza Ndanda amefariki dunia baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa tumbo. … Read More
0 comments:
Post a Comment