Monday, April 25, 2016

Yanga Kufanya Uchaguzi Tarehe Hii Hapa


Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) leo imetangaza Juni 05, 2016 kuwa siku ya Uchaguzi Mkuu wa viongozi ndani ya klabu ya Young Africans SC ya jijini Dar es salaam.

Akiongea na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi TFF, Wakili Aloyce Komba amesema mchakato mzima wa uchaguzi wa klabu ya Young Africans utakuwa ndani ya siku 33, ambapo mchakato unatarajiwa kuanza rasmi Mei 03, 2016.

Komba amesema jukumu lao Kamati ya Uchaguzi TFF  ni kusimamia na kuhakikisha Uchaguzi Mkuu wa klabu hiyo unafanyika katika hali ya demokrasia.

Ifuatayo ni kalenda ya mchakato wa Uchaguzi katika klabu ya Young Africans SC:

Mei 03, 2016 Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi TFF, atatangaza mchakato wa kulabu ya Young Africans, nafasi zinazogombewa na kubandika kwenye mbao za matangazo.

Mei 04-9, 2016 – Kuanza kuchukua fomu za kugombea na mwisho wa kurudisha fomu kwa wagombea.

Mei 10, 2016 Kamati ya Uchaguzi TFF itakaa kikao cha mchujo wa awali  wa wagombea na kuandika barua za kuwajulisha wagombea juu ya mchujo wa awali.

Mei 11, 2016 Kamati ya Uchaguzi TFF itachapisha na kubandika kwenye mbao za matangazo orodha ya awali ya wagombea.

Mei 12-13, 2016 Kipindi cha kupokea na kuweka pingamizi kwa wagombea wote.

Mei 14-15, 2016 Kamagi ya Uchaguzi TFF itapitia pingamizi zote na kufanya usajili wa wagombea.

Mei 16, 2016 Kamati ya Uchaguzi TFF itatangaza na kubandika kwenye mbao za matangazo matokeo ya awali ya usahili.

Mei 17, 2016 Sekretarieti kuwasilisha masuala ya kimaadili kwenye Kamati ya Maadili ya TFF.

Mei 18-19, 2016 Kamati ya Maadili TFF itapokea, kusikiliza na kutolea maamuzi ya kamati ya maadili.

Mei 20, 2016 Kamati ya Maadili ya TFF itatangaza maamuzi ya kamati.

Mei 21-22, 2016 Kipindi cha kukata Rufaa kwa maamuzi ya masuala ya Kimaadili kwenye kamati ya Rufaa ya Maadili TFF.

Mei 23, 2016 Kamati ya Maadili tff itasikiliza rufaa za kimaadili.

Mei 24, 2016 Kamati ya Rufaa ya Maadili itatoa maamuzi ya Rufaa.

Mei 25-26, 2016 Kipindi cha kukata Rufaa dhidi ya Kamati ya Uchaguzi kwenye kamati ya Rufaa ya Uchaguzi TFF.

Mei 27-28, 2016 Rufaa kusikilizwa na kamati ya Rufaa ya Uchaguzi ya TFF.

Mei 29, 2016 Kamati ya Rufaa ya Uchaguzi TFF kutangaza maamuzi ya Kamati ya Uchaguzi ya TFF.

Mei 30, 2016 Kamati ya Uchaguzi TFF kuchapisha orodha ya mwisho ya wagombea na kutangazwa na kubandikwa kwenye mbao za matangazo.

Mei 31 – Juni 04, Kipindi cha kampeni kwa wagombea.

Juni 05, 2016 siku ya Uchaguzi Mkuu wa klabu ya Young Africans.

Wakati huo huo Kamati ya Rufaa ya TFF Jumamosi, itasikiliza pia rufaa ya klabu ya Geita Gold pamoja na rufaa ya kocha msaidizi wa Toto Africans Choke Abeid,



Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

Related Posts:

  • TFF YAZIKUMBUSHA TENA KLABU ZA LIGI KUU 2016/17 Kwa mara nyingine, Bodi ya Ligi Kuu ya Shirikisho la Soka (TFF) imezikumbusha klabu zitakazoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2016/17 kuwa mchakato wa wa utengenezaji kanuni umeanza tangu Mei 5, 2016. Bodi ya Ligi… Read More
  • YANGA BINGWA TENA 2015/16 MCHEZO Kati ya Simba SC na Mwadui FC umemalizika kwa Mwadui kuibuka na ushindi wa goli 1 - 0. Simba walikuwa wanahitaji kushinda katika mechi hii ili kuisubirisha Yanga kutangaza ubingwa mapema, lakini hilo limeshindikan… Read More
  • SIMBA YAIFUATA MAJIMAJI SONGEA Kikosi cha Simba kimesafiri alfajiri ya leo kuelekea Songea tayari kwa mchezo wake dhidi ya Majimaji FC. Simba itaingia katika mchezo huu ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo wake wa awali dhidi ya Mwadui FC, hivyo kuh… Read More
  • SIMBA SC WAIDUNGUA MTIBWA SUGAR NYUMBANI KWAO SIMBA ilishuka dimbani hivi leo kucheza na Mtibwa Sugar katika mchezo wao wa 29 wa ligi kuu Tanzania bara,Mchezo uliopigwa mjini Morogoro. Mchezo huo umemalizika kwa Simba SC kushinda kwa goli 1 - 0 goli lililofungwa na… Read More
  • YANGA WAKABIDHIWA RASMI KOMBE LAO KLABU Ya Yanga imekabidhiwa kombe lao jioni ya leo katika uwanja wa taifa mara tu baada ya kumalizika kwa mchezo wao dhidi ya Ndanda FC, mchezo ambao umemalizika kwa sare ya 2 - 2. Ndanda FC ndio walikuwa wa kwanza kupata… Read More

0 comments:

Post a Comment