Tuesday, April 26, 2016

Farid Mussa Aanza Majaribio La Liga


WINGA machachari wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Farid Mussa, ameanza majaribio rasmi nchini Hispania akiwa na kikosi cha timu ya CD Tenerife inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza nchini humo.

Farid, 20, aliyefika juzi nchini humo akitokea Tunisia, Azam FC ilipokwenda kucheza na Esperance ya huko kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika, ambapo usiku wa kuamkia leo alitarajiwa kuwa miongoni mwa wachezaji wa Tenerife watakaocheza mchezo wa kirafiki na moja ya timu ya Ligi Daraja la Kwanza huko.

Akizungumza na mtandao rasmi wa klabu www.azamfc.co.tz kutoka nchini humo Farid alisema benchi la ufundi la Tenerife lilipanga kumpa dakika 45 za kucheza ili kuonyesha uwezo wake kwenye mchezo huo ikiwa ni sehemu ya majaribio pia.

“Namshukuru Mungu wamenipokea vizuri na wameonyesha kunikubali, kiufupi naendelea vizuri sana huku na usiku wa leo (jana) nitaanza kwa kucheza mchezo wa kirafiki kwa dakika 45, nimejipanga kufanya vema katika sehemu yangu ya majaribio huku ili niweze kubakia huku na kuitangaza timu yangu ya Azam FC,” alisema.

Nyota huyo chipukizi aliyekuzwa na kituo cha kulea vipaji cha Azam FC ‘Azam FC Academy’, alimalizia kwa kusema kuwa kwa mujibu wa wakala wake John Sorzano raia wa Venezuela aliyeishi sana nchini England, amedai kuwa wiki ijayo anatarajia kuanza rasmi majaribio katika timu mbili za Ligi Kuu Hispania ‘La Liga’ akianzia Las Palmas na kumalizia Malaga.

Farid atafanya majaribio hayo na kukaa huko kwa takribani wiki tatu na anatarajia kurejea nchini Mei 19 mwaka huu, hiyo inamaanisha kuwa atakosa mechi zote za Azam FC zilizobakia za msimu huu.

Lakini mechi pekee ambayo anaweza kuiwahi ni ile ya fainali ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) itakayofanyika Mei 25 mwaka huu, ambayo Azam FC ilitinga juzi kwa kuichapa Mwadui ya Shinyanga na itacheza na mshindi wa nusu fainali nyingine kati ya Yanga na Coastal Union.   

Chanzo: Azam Fc Official Site




Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

Related Posts:

  • AZAM FC YAICHAPA AFRICAN SPORTS Klabu Bingwa Afrika Mashariki na kati Azam FC ilikuwa ugenini jijini Tanga kupambana na African Sports katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom. Azam FC wamefanikiwa kuibuka na ushindi katika mchezo h… Read More
  • SIMBA SC WAIDUNGUA MTIBWA SUGAR NYUMBANI KWAO SIMBA ilishuka dimbani hivi leo kucheza na Mtibwa Sugar katika mchezo wao wa 29 wa ligi kuu Tanzania bara,Mchezo uliopigwa mjini Morogoro. Mchezo huo umemalizika kwa Simba SC kushinda kwa goli 1 - 0 goli lililofungwa na… Read More
  • VITA YA KUWANIA NAFASI YA PILI VPL KUENDELEA TENA LEO LIGI kuu Tanzania bara inatarajia kuendelea tena leo katika viwanja viwili. Mjini Morogoro wakata miwa wa Mtibwa watawakaribisha vijana wa Msimbazi Simba SC wakati huko Tanga Azam FC itachuana na African Sports. Simba w… Read More
  • MBEYA CITY, YANGA KUSIMAMISHA JIJI LEO Ligi kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom inatarajiwa kuendelea tena leo kwa mchezo  utakaowakutanisha Mbeya City ya Jijini Mbeya dhidi ya Yanga ya  jijini Dar-Es-Salaam. Yanga inaingia katika mchezo huu … Read More
  • NDANDA FC WAPANIA KUHARIBU SHEREHE YA YANGA Msemaji wa klabu ya Ndanda FC Idrisa Bandari amesema watahakikisha wanaifunga Yanga na kuharibu Sherehe yao ya kukabidhiwa kombe leo katika mchezo utakaopigwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar. Yanga wanaingia katika mc… Read More

0 comments:

Post a Comment