Friday, April 29, 2016

BREAKING NEWS: BODI YA EVERTON KUJADILI HATIMA YA MARTINEZ LEO



Klabu ya Everton ipo tayari kukaa kikao leo na kujadili hatima ya kocha wa timu hiyo Roberto Martinez.
Martinez amezungumza jana kuwa Bodi ya Everton iko sahihi kujadili hatima yake kufuatia mwenendo mbovu wa timu hiyo.

Everton ambayo inacheza na Bournemouth wikiendi hii imekuwa na msimu mbovu wakiwa wanashika nafasi ya 11 katika msimamo wa ligi. Kiwango kibovu kinachoonyeshwa hasa katika uwanja wa nyumbani ndo limekuwa suala kubwa sana ambalo linawaumiza mashabiki, wakiwa wameshinda michezo 4 tu katika uwanja wao wa Goodison kitu ambacho kinamfanya Martinez kuwa katika wakati mgumu klabuni hapo.


Martinez ambae alikuwa na misimu mizuri sana katika klabu za Swansea City na Wigan Athletic kabla hajajiunga na Everton ni wazi kuwa ataonyeshwa mlango wa kutokea na wamiliki wa timu hiyo Farhad Moshiri na mwenyekiti Bill Kenwright sambamba na jopo zima la bodi ya timu hiyo kufuatia kiwango kibovu cha timu hiyo iliyochini ya Mhispania huyo mwenye umri wa miaka 42.

Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

0 comments:

Post a Comment