Wednesday, November 9, 2016

MCHEZO WA YANGA NA RUVU SHOOTINGI WASOGEZWA MBELE SIKU MOJA


Wakati ligi kuu ikiendelea leo jumatano, mchezo mmoja kati ya Yanga na Ruvu Shooting umesogezwa mbele hadi kesho alhamisi Kutokana na kuchelewa kuwasili kwa timu ya Ruvu katika kituo cha Dar es salaam ikitokea mkoani Kagera ilipokuwa imecheza mchezo wake wa raundi ya 14 dhidi ya wenyeji wao Kagera sugar.

Michezo mingine miwili inaendelea kama ilivyopangwa siku ya leo, Tanzania Prisons itaikaribisha Simba huko Mbeya wakati huohuo huko Shinyanga wenyeji Mwadui wataikaribisha Azam ya Dar es salaam.

0 comments:

Post a Comment