Thursday, July 7, 2016

YANGA SASA KUKIONA CHA MOTO

Klabu ya Yanga ipo hatarini kuburuzwa katika mahakama ya kibiashara na wadhamini wao kampuni ya Bia Tanzania (TBL).

Yanga Huenda ikafikishwa mahakamani kwa kile kinachodaiwa kuvunja mkataba na wadhamini wao kampuni ya TBL.

Habari zaidi zinasema TBL inakusudia kuipeleka Yanga Mahakaman kutokana na kushindwa kutimiza makubaliano ya mkataba wao.

"Hatua ya makundi ambayo Yanga wamefika ilikuwa ni muhimu sana kwa mdhamini wao kumtangaza, lakini badala yake wameingia hatua hiyo wameondoa nembo ya mdhamini wao , wakati bado wapo ndani ya mkataba, hivyo TBL inapanga kuipeleka Yanga katika mahakama ya Biashara, mwezi mmoja uliobaki ulikuwa na manufaa zaidi kwa wadhamini na maana kubwa kuliko kipindi chote ambacho wamewadhamini" alisema Ofisa kutoka katika kampuni hiyo ya TBL.

Ofisa huyo aliongeza kuwa kinachoshangaza zaidi ni kwamba Yanga wameenda Algeria wameondoa nembo ya mdhamini kifuani, na kwamba siku za hivi karibuni wamekuwa na maelewano ambayo sio mazuri na mdhamini huyo.

Hata hivyo Yanga haijatangaza rasmi kuvunja mkataba na TBL lakini tayari wameanza kuutumia mkataba wa Quality Group Limited inayomilikiwa na Yusuf Manji mwenyekiti wa klabu hiyo.

Aidha Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Yusuf Manji kupitia tarifa yake ya hivi karibuni amesema kuwa mkataba wa Yanga na TBL uliosainiwa miaka mitano iliyopita na mtangulizi wake (Mwenyekiti aliyepita) ulikuwa ni haramu, kwani mamlaka ya kutia saini kwa mujibu wa katiba ya Yanga yapo kwa bodi ya wadhamini.
Bonyeza Hapa Ku-Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook



Related Posts:

  • Yanga Na Azam Fc Zasusia Ratiba Kombe La FA Hili ndo Kombe La ASFC Yanga na Azam Fc zimesusia Ratiba ya michuano ya Azam Sports Federation Cup hatua ya nusu fainali iliyopangwa kufanyika  April 24 mwaka huu. Timu zote zimetoa sababu ya kushiriki michuano ya kum… Read More
  • Kiiza, Juuko Murshid Kikaangoni Msimbazi Tayari Simba wameanza kuangushiana lawama za chinichini. Jambo ambalo si sahihi lakini wapo ambao walikuwa chanzo cha kuua umoja katika mechi hiyo au kutokuwa makini, kukachangia wao kung’oka. Kiiza&Juuko kikaangoni:… Read More
  • Afya Ya Kapombe Yazidi Kuimarika BEKI kisiki wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Shomari Kapombe, anaendelea vema na matibabu nchini Afrika Kusini huku ikielezwa kuwa afya yake inazidi kuimarika kadiri siku zinavyosogea. Kapombe yupo jiji… Read More
  • Yanga Na Mwadui, Azam FC Na Mtibwa Michuano ya Ligi kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom Premier League ( VPL ) inatarajiwa kuendelea tena hapo kesho kwa mechi mbili. Yanga iliyotoka kumenyana na Al Ahly juzi itawakaribisha vijana wa Jamhuri Kiwelu Julio … Read More
  • Kombe La FA Ngoma nzito.... Angalia matokeo ya droo hapa.Droo ya michuano ya Kombe la Shirikisho hatua ya nusu fainali, leo imepangwa. Mwadui FC imepangiwa Azam FC na mechi ya kwanza itachezwa mjini Shinyanga wakati Yanga wao watacheza na Coastal Union ambao wataanzia mjini Tanga. … Read More

0 comments:

Post a Comment