Monday, April 25, 2016

Simba Yaendelea Kujifua Huko Visiwani Zanzibar



Timu ya Simba Sports Club imeendelea na mazoezi tena leo huko visiwani Zanzibar yakiwa ni maandalizi dhidi ya mchezo wao na Azam FC.
Simba ambao kwa mechi za hivi karibuni wamekuwa hawafanyi vizuri wameelekea visiwani Zanzibar kujiandaa na mchezo huo muhimu zaidi kwao kwani msimamo wa ligi bado unawapa nafasi ya kupigania ubingwa wa ligi kuu Bara Msimu huu. Kwa takribani miaka mitatu sasa hivi Simba hawajashiriki mashindano ya kimataifa kitu ambacho kinawanyima usingizi sio tu viongozi wa klabu hiyo bali pia Mashabiki na wapenzi wa Simba wanaumia kuona timu yao inakosa kushiriki michuano ya Kimataifa.

Simba wanahitaji ushindi ili kuongeza presha kwa Yanga wanaoshika nafasi ya kwanza katika msimamo huo wakiwa wamewaacha Simba kwa pointi mbili tu. Msimamo wa ligi jinsi ulivyo timu yoyote kati ya Simba, Yanga na Azam FC inaweza kuibuka bingwa wa Msimu huu kwani timu hizi zinatofautina kwa pointi chache sana.

Kutokana na kuanzishwa kwa kombe la shirikisho (FA) timu itakayochukua nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kuu haitashiriki katika mashindano ya kimataifa kama ambavyo ilikuwa inafanywa hapo mwanzo badala yake mshindi wa kombe la FA ndiye atakaeshiriki mashindano ya kimataifa pamoja na mshindi wa ligi kuu Bara. Simba iliondoshwa katika michuano ya FA wiki moja iliyopita baada ya kukubali kipigo cha goli 1 - 0 kutoka kwa Coastal Union mechi iliyochezwa uwanja wa Taifa hivyo kuifanya Simba kuelekeza nguvu zao zote katika Ligi Kuu Tanzania Bara ambako wananafasi ya kuchukua ubingwa endapo watafanya vizuri katika mechi zao zote zilizobaki huku wakiwaombea wapinzani wao kupoteza japo mechi moja huku wao wakishinda mechi zote ambapo watamaliza ligi wakiwa mbele kwa tofauti ya pointi moja.

Simba wanahitaji utulivu na kuondosha tofauti katika klabu yao na kuongeza hamasa kwa wachezaji ili waweze kufanya vizuri na hatimaye kuibuka mabingwa.









pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.com

Related Posts:

  • MBEYA CITY, YANGA KUSIMAMISHA JIJI LEO Ligi kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom inatarajiwa kuendelea tena leo kwa mchezo  utakaowakutanisha Mbeya City ya Jijini Mbeya dhidi ya Yanga ya  jijini Dar-Es-Salaam. Yanga inaingia katika mchezo huu … Read More
  • NDANDA FC WAPANIA KUHARIBU SHEREHE YA YANGA Msemaji wa klabu ya Ndanda FC Idrisa Bandari amesema watahakikisha wanaifunga Yanga na kuharibu Sherehe yao ya kukabidhiwa kombe leo katika mchezo utakaopigwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar. Yanga wanaingia katika mc… Read More
  • VICENT BOSSOU AITWA TIMU YA TAIFA YA TOGO Kocha mpya wa Togo Mfaransa Claude LeRoy amemuita Vicent Bossou katika kikosi cha timu yake ya Taifa .Bossou ameitwa kutokana na kiwango kizuri alichokionyesha akiwa na klabu ya Yanga. Tayari barua ya mualiko wa kujiu… Read More
  • VITA YA KUWANIA NAFASI YA PILI VPL KUENDELEA TENA LEO LIGI kuu Tanzania bara inatarajia kuendelea tena leo katika viwanja viwili. Mjini Morogoro wakata miwa wa Mtibwa watawakaribisha vijana wa Msimbazi Simba SC wakati huko Tanga Azam FC itachuana na African Sports. Simba w… Read More
  • AMIS TAMBWE AMWOMBEA MABAYA KIIZA MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Dar Young Africans Amis Tambwe, amemaliza mchezo wa jana dhidi ya Ndanda FC bila ya kufunga goli, Tambwe anayeongoza katika orodha ya wafungaji bora katika ligi kuu Tanzania bara msim… Read More

0 comments:

Post a Comment