Yanga Yainyoosha Azam Fc Chamanzi

Azam FC 1 - 2 Young Africans.

Kiungo Wa Everton James McCathy Avunjika Mguu

Kiungo James McCarthy wa Everton sasa atakaa nje na kuukosa msimu wote huh baada ya kuvunjika mifupa miwili ya mguu wake.

DRAW CAF CL And CC 2018

Draw Caf Cl and CC 2018

Yanga Yazinduka Yaambulia Ushindi Mwembamba

Klabu ya Yanga leo imefanikiwa kuibuka na ushindi mwembamba wa goli moja kwa sifuri

Madrid Yaivurumisha Deportivo 7-1

Klabu ya Real Madrid leo imefanikiwa kuchomoza na ushindi mnono kwa jumla ya magoli 7-1 dhidi ya Klabu Deportivo la Coruna

Showing posts with label Azam Sports Federation Cup. Show all posts
Showing posts with label Azam Sports Federation Cup. Show all posts

Tuesday, March 7, 2017

Ratiba robo fainali Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup)



Ratiba hiyo iliyotelewa mapema leo imepangwa kama ifuatvyo:

March 18 Madini fc wataikaribisha Simba Sc katika dimba la Sheikh Amri Abeid, Arusha, siku hiyohiyo ya Tarehe march 18 Kagera Sugar itaialika Mbao ndani ya Uwanja wa Kaitaba, mjini Bukoba.

Michezo miwili iliyobaki ni kati ya Azam FC watakapoikaribisha Ndanda fc toka Mtwara katika dimba la chamanzi.

Yanga wataikaribisha Tanzania Prisons katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Michezo kati ya Azam na Ndanda, Yanga na Prisons haijapangiwa ni lini itafanyika Kutokana na Yanga kushiriki michuano ya kilabu bingwa barani Afrika huku Azam wao wakishiriki michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika.


Mshindi wa michuano hiyo kikanuni anatarajia kujishindia kombe pamoja na kitita cha Sh. milioni 50 na kuiwakilisha Tanzania Bara kwenye Kombe la Shirikisho Afrika mwakani.
Madini vs Simba 
Kagera vs Mbao
Yanga vs Prisons
Azam vs Ndanda

Monday, March 6, 2017

Yanga vs Kiluvya fc kesho Taifa 16 bora ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Sports Federation Cup)


Kilvya na Yanga kesho kuamua ni timu gani iingie robo fainali kuungana na timu saba ambazo zimefuzu kwa hatua hiyo.

Bingwa wa michuano hii ndie anaeiwakilisha nchi katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika, pia hujinyakulia kitita cha shilingi milion 50 za kitanzania.


Timu saba ambazo zimefuzu kwa hatua ya robo fainali ni Tanzania Prisons ya Mbeya, Ndanda FC ya Mtwara, Azam FC ya Dar es Salaam, Madini ya Arusha, Simba ya Dar es Salaam, Mbao FC ya Mwanza, Kagera Sugar ya Bukoba.

Monday, February 6, 2017

16 Bora Azam Federation Cup ratiba yatangazwa, michezo 8 kufanyika kwa siku tatu tofauti


Michuano ya kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) hatua ya 16 bora kutimua vumbi February 24 na February 26 na march 7 katika mikoa sita ya Tanzania Bara.
February 24 kutakuwa na michezo minne katika mikoa minne tofauti
Mkoani Arusha
Katika dimba la Sheikh Amri Abeid wenyeji timu ya Madini Fc watawakaribisha maafande wa JKT Ruvu
Mkoani Dar es Salaam
Mabingwa wa Afrika Mashariki na kati Azam Fc watailika timu ngumu ya Mtibwa Sugar katika dimba lao la nyumbani (Azam Complex, Chamaz).
Azam  ndio makamu bingwa wa michuano hiyo kwa msimu uliopita baada ya kupokea kichapo cha goli 3 – 1 kutoka kwa Yanga.

Mkoani Kagera

Timu ya Kagera sugar wataikaribisha timu ya Stand United katika dimba Kaitaba.

Mkoani Ruvuma

Timu za Mighty Elephant mkoani humo itawaalika wanakuchele Ndanda kutoka Mtwara katika Uwanja wa Majimaji mjini Songea.
Raundi hiyo ya 16 itaendelea tena siku ya jumapili February 26 katika mikoa mitatu.
Mkoani Dar es Salaam

Timu ya Simba itavaana na timu African Lyon katika dimba la Uwanja wa Taifa.

Mkoani Mwanza

Kutakuwa na Mwanza derby wakati Mbao FC itakapoonyeshana ubabe na kaka zao Toto Africans katika Uwanja wa CCM Kirumba
Mkoani Mbeya

Derby nyingine itakuwa mkoani Mbeya wakati timu mbili za mkoani humo Tanzania Prisons na Mbeya City zitakapomenyana kuwania kuingia roba fainali ya michuano hiyo

March 7


Mabingwa wa michuano hiyo kwa msimu uliopita timu ya Yanga wao wataialika timu ya Kiluvya kutoka mkoani pwani katika dimba kuu la Uwanja wa Taifa jiji Dar es Salaam

bingwa wa michuano hii ndie atakaeiwakilisha Tanzania katika michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika 2018.

Thursday, January 26, 2017

Rufaa ya polisi Dar es Salaam dhidi ya mchezaji wa simba Novalty Lufunga kucheza huku akiwa na kadi nyekundu yagonga mwamba


Shirikisho la mpira wa miguu nchini Tanzania limeitupilia mbali rufaa ya timu ya polisi Dar es salaam waliokata kutaka wapewe ushindi katika mchezo wao wa raundi ya tano  ambao simba ilishinda kwa 2 -0,

Mchezaji Novalty Lufunga aliekatiwa rufaa alipata kadi nyekundu katika mchezo wa mwisho kwa simba wa  Azam Sports Federation Cup 2015/2016 ambapo simba ililala katika mchezo huo wa 11april 2016 kuondoshwa mashindanoni.

Kanuni za  Azam Sports Federation Cup zinaweka wazi kuwa kadi ya njano au nyekundu inaisha pale tu mashindano husika yanapoisha labda itokee kadi hiyo imeongezewa na adhabu nyingine, kama itakuwa imeongezewa adhabu basi klabu na mchezaji watataarifiwa  kwa maandishi.

Hivyo basi kwa kanuni hiyo ya mashindano polisi Dar itakuwa imetupwa nje rasmi katika mashindano hao ya Azam Sports Federation Cup