Wednesday, June 22, 2016

TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO JUMATANO JUNI 22,2016

Tetesi Za Usajili Barani Ulaya

 Bale Kupewa Mkataba Mrefu Madrid
Mchezaji wa kimataifa wa Wales, Gareth Bale anatarajiwa kupewa mkataba mpya utakaomuweka Santiago Bernabeu Kwa zaidi ya miaka 6.

Barcelona Yamuwinda Gabriel Jesus
Jesus 19, anawindwa na mabingwa wa La Liga, Barcelona na Mabingwa hao wamekuwa wakimfuatilia kwa karibu katika mechi zake anazocheza kwenye klabu yake ya Palmeiras.


Rasmi: Morata Asaini Real Madrid
Morata 23, amekuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na mabingwa hao wa Uefa Champions League mara 11 akitokea Jeventus kwa uhamisho wa paundi milioni 32.


Lukaku Hana Haraka Ya Kuondoka Everton
Wakala wa Mshambuliaji huyo amesema Chelsea watakumbana na changamoto nzito katika harakati zao za kutaka kunasa saini ya Lukaku, kwani bado anahitaji kubaki Everton.

Leicester City Kumsainisha Hernandez
Hernandez atajiunga na Leicester City kwa mkataba wa miaka wa minne kwa mujibu wa mabingwa hao wa ligi kuu ya Uingereza msimu wa 2015/16

Redknapp Asema West Ham Haitamuuza Payet
Wagonga nyundo hao wameweka kiwango cha paundi milioni 60 kwa klabu itakayohitaji kumsajili Payet, Hata hivyo Redknapp amesema hawana mpango wa kumuuza mchezaji huyo anayefanya vizuri katika michuano ya Euro inayoendelea huko nchini Ufaransa.

0 comments:

Post a Comment