Thursday, June 23, 2016

SUALA LA YANGA KUTAKA MECHI NA MAZEMBE ISOGEZWE MBELE

TFF imesema kuwa imepokea maombi ya Yanga ya kutaka shirikisho hilo kuiandikia CAF wakitaka mchezo wao wa Kombe la Shirikisho la Soka la Afrika(CAF-CC) dhidi ya TP Mazembe uchezwe Juni 29 badala ya Juni 28.

“Yanga walipewa nafasi ya kuchagua tarehe tatu za mchezo huo kufanyika ambapo ni tarehe 28, 29 na 30 na CAF na walitakiwa wachague moja ya tarehe hizo na kuthibitisha CAF, lakini hawakufanya hivyo na CAF kuamua mechi hiyo ichezwe tarehe 28 saa 10:00 jioni. “Sasa wamekuja wakitaka tuwasaidie kuwaombea CAF ili mchezo wao uchezwe Juni 29 saa 7:30 usiku kwa hoja ya kutoa nafasi kwa baadhi ya mashabiki wao ambao baadhi yao ni waumini wa dini ya Kiislamu kuweza kushuhudia mechi hiyo na tayari tumeshawaandikia CAF na tunasubiri majibu yao,” alisema Lucas Ofisa Habari wa TFF.

Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook Hapa

0 comments:

Post a Comment