Friday, June 24, 2016

JKT OLJORO YAMIMINIWA MAMILIONI

Timu ya maafande wa JKT Oljoro ya jijini Arusha inayojiandaa na michuano ya ligi daraja la pili (SDL) msimu wa 2016/17 imekabidhiwa vifaa vya michezo vyenye thamani ya Shi. Milioni 3.4 kutoka kwa kampuni ya Sanlam.

Vifaa hivyo ni pamoja na Jozi 30, Jezi za mazoezi Jozi 30, soksi za michezo na kofia za jua.
Meneja kanda za juu kaskazini kutoka katika kampuni hiyo, Charles Mwamulenga alisema vifaa hivyo vimekabidhiwa kwa timu hiyo ikiwa ni moja ya kuwaunga mkono katika mashindao yanayowakabili.

Amos Mwita aliyepokea vifaa hivyo kwa niaba ya mkuu wa kikosi cha Jeshi 833 Oljoro, amesema wanashukuru kampuni hiyo kwa moyo waliouonyesha kwa timu yao na kwamba ni wakati sasa umefika kwa timu hiyo kujipanga ili iweze kufanya vizuri.

"Kama timu hivi sasa itawekeza hamasa yake katika maadalizi ya hali ya juu vile vile itahakikisha inatoa hamasa kwa wapenzi wa soka Arusha ili kuiunga mkono iweze kusonga mbele katika michuano inayoikabili ya SDL" alisema Mwita.

Aidha katibu mkuu wa timu hiyo, Hussein Nalinga amesema kuwa tayari timu yao imeanza kambi kwa takribani wiki mbili sasa na kwamba matarajio yao ni kufanya vizuri.

Like Ukurasa Wa Soka24 Facebook Hapa

Related Posts:

  • HASSAN RAMADHANI KESSY AMWAGA WINO YANGA Beki wa kulia wa Simba SC, Hassan Ramadhani Kessy (katikati) akitia dole gumba kwenye fomu za Mkataba wa Yanga, Kessy amesaini miaka miwili kuitumikia Yanga kuanzia mwezi ujao. Zoezi hilo lilifanyika juzi usiku mjini Dar… Read More
  • SIMBA YAIFUATA MAJIMAJI SONGEA Kikosi cha Simba kimesafiri alfajiri ya leo kuelekea Songea tayari kwa mchezo wake dhidi ya Majimaji FC. Simba itaingia katika mchezo huu ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo wake wa awali dhidi ya Mwadui FC, hivyo kuh… Read More
  • HIKI NDO KIKOSI CHA SERENGETI BOYS Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi amewataka wachezaji wa timu ya soka ya vijana wa Tanzania wenye umri wa chini ya miaka 17 maarufu kama jina la Serengeti Boys kwenda kucheza soka la ushi… Read More
  • TFF YAZIKUMBUSHA TENA KLABU ZA LIGI KUU 2016/17 Kwa mara nyingine, Bodi ya Ligi Kuu ya Shirikisho la Soka (TFF) imezikumbusha klabu zitakazoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom msimu wa 2016/17 kuwa mchakato wa wa utengenezaji kanuni umeanza tangu Mei 5, 2016. Bodi ya Ligi… Read More
  • RATIBA YA FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO (ASFC) Fainali za kuwania Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) sasa zitafanyika Juni 11, 2016. Mchezo huo wa fainali utakaozikutanisha timu za soka ya Young Africans na Azam… Read More

0 comments:

Post a Comment