Yanga Yainyoosha Azam Fc Chamanzi

Azam FC 1 - 2 Young Africans.

Saturday, April 30, 2016

YANGA YAZIDI KUCHANJA MBUGA KAZI IMEBAKI KWA AZAM NA SIMBA

LIGI Kuu Tanzania Bara imeendelea tena hivi leo katika viwanja 4, huko Jijini Mwanza wenyeji Toto Africans Wakiikaribisha Yanga. Mchezo huo ulioshuhudiwa na maelfu ya watazamaji ulikuwa na wa kuvutia ukizingatia kwamba timu hizo mbili licha ya kuhusishwa na undugu leo ziliingia uwanjani kila moja ikihitaji ushindi katika mchezo huo. Toto ndo walikuwa wa kwanza kupata goli kipindi cha kwanza cha mchezo dakika ya 39 goli lililofungwa na William...

LIVE KUTOKA MWANZA: TOTO VS YANGA

Ligi Kuu Tanzania Bara FULL TIME Toto 1-2 Yanga W.Kimanzi Tambwe, J. Abdul AFrican SC 1 - 0 Coastal Live Updates Kupitia soka24.blogspot.com Pata habari za michezo kwa haraka zaidi kupitia soka24.blogspot.co...

ANTONIO CONTE AKUBALI KUMUUZA STAA HUYU KWA PAUNDI ML. 50

KOCHA mpya wa Chelsea Antonio Conte licha ya kuwa anapenda kuwaacha mastaa wake wote katika kikosi hicho na alishaitisha kikao na timu kuliweka wazi suala hilo, amekubali kuwa licha ya kukosa nafasi ya kucheza klabu bingwa ulaya atapambana kuhakikisha anabakisha mastaa wake wote klabuni hapo.  Kufuatia kuondoka kwa John Terry wachezaji wengine ambao nao wapo mbioni kuondoka klabuni hapo ni pamoja na Eden Hazard, Diego Costa, Willian...

KIKOSI CHA YANGA LEO DHIDI YA TOTO AFRICANS

KIKOSI CHA YANGA LEO. 1. Deogratius Munishi Dida. 2. Juma Abdul Japhary. 3. Oscar Fanuel Joshua. 4. Kelvin Patrick Yondani. 5. Vicent Bossou. 6. Salum Abo Telela. 7. Saimon Happygod Msuva. 8. Haruna Fadhil Niyonzima. 9. Amiss Jocelyn Tambwe. 10. Donald Dombo Ngoma. 11. Deus David Kaseke. BENCHI. Ally Mustafa Mtinge. Haji Mwinyi Ngwali. Mbuyu Junior Twite. Nadir Haroub Ally. Malimi Marcel Busungu. Thaban Michael Kamusoko. Matheo...

HUU NDIO USAJILI WA KWANZA WA MOURINHO MAN UTD

MANCHESTER United wamekubali kulipa ada ya uhamisho ya Euro Milion 80 ili kumnasa nyota wa Benifica Renato Sanches. Gazeti la Michezo la Ureno limeripoti kuwa katika dili hilo Man Utd watalazimika kulipa Euro Milioni 40 Cash na 40 itakayobakia italipwa baadae. Usajili huo umepata mitazamo tofauti huku wataalamu wa soka wakisema ni kiwango kikubwa sana cha pesa alichosajiliwa Renato ukizingatia bado hajadhihirisha ubora wake kiasi cha kumnunua...

Friday, April 29, 2016

SIMON MIGNOLET HATARINI KUTIMULIWA LIVERPOOL

Mlinda mlango wa Liverpool  Simon Mignolet ameonekana kuwaangusha mamilioni ya mashabiki wa Liverpool msimu huu na kocha Klopp anafikiria kumleta kipa mwingine anayechezea Barcelona kwa sasa Marc-Andre ter Stegen. Mlinda mlango huyo wa Barcelona anayesifiwa sana kwa kiwango chake alichoonyesha klabuni hapo tangu alipojiunga mwaka 2014, amekuwa katika mipango ya Jurgen Klopp ili kuimarisha kikosi chake katika nafasi hiyo ya mlinda mlango. Alipoulizwa...

LOUIS VAN GAAL ANAAMINI BADO ANA NAFASI YA KUBAKI MAN UTD

Louis Van Gaal bado anaamini anaweza akatetea kibarua chake kwa kushinda kombe la FA na kumaliza katika nafasi ya Nne katika msimamo wa  ligi kuu nchini England-EPL. Matumaini ya  Mdachi huyo kumaliza mkataba wake ambao umebakisha mwaka mmoja klabuni hapo yamekuwa ni madogo kutokana na matokea mabaya ya klabu hiyo na mbinu mbovu zinazolalamikiwa na mashabiki wa klabu hiyo. Kwa upande mungine kambi ya Jose Mourinho inaamini kuwa Mreno...

RUFAA YA MICHEL PLATINI KUTOLEWA MAAMUZI MAPEMA WIKI IJAYO

ALIYEKUWA Rais wa UEFA Michel Platini ameonekana mbele ya waandishi wa habari ijumaa hii katika mahakama inayojishugulikia usuluhishi wa masuala ya michezo, kupinga kifungo alichopewa cha miaka 6 ya kutojihusisha na masuala ya Mpira wa miguu akisema ana uhakika wa kushinda rufaa hiyo, Sepp Blatter rais wa Zamani wa Fifa akiwa miongoni mwa mashahidi wake. Platini aliyeletwa na na taxi katika mahakama hiyo ya usuluhishi wa masuala ya michezo...

LIVERPOOL YASHINDWA KUTAMBA MBELE YA VILLARREAL

KIKOSI Cha Liverpool chini ya kocha Mjerumani Jurgen Klopp kimeshindwa kuendeleza ubabe mbele ya klabu ya Villarreal kutoka nchini Hispania katika mechi ya kwanza ya Hatua ya Nusu fainali Europa League. Klabu ya Villarreal ambayo imeshinda mechi zote za mashindao hayo msimu huu katika uwanja wa nyumbani huku wakiruhusu kufungwa mara moja tu katika dimba hilo la Estadio El Madrigal, ilipata ushindi huo baada ya goli lililofungwa dakika ya 92...

BREAKING NEWS: BODI YA EVERTON KUJADILI HATIMA YA MARTINEZ LEO

Klabu ya Everton ipo tayari kukaa kikao leo na kujadili hatima ya kocha wa timu hiyo Roberto Martinez. Martinez amezungumza jana kuwa Bodi ya Everton iko sahihi kujadili hatima yake kufuatia mwenendo mbovu wa timu hiyo. Everton ambayo inacheza na Bournemouth wikiendi hii imekuwa na msimu mbovu wakiwa wanashika nafasi ya 11 katika msimamo wa ligi. Kiwango kibovu kinachoonyeshwa hasa katika uwanja wa nyumbani ndo limekuwa suala kubwa sana ambalo...

TCHETCHE YUKO FITI KUIVAA SIMBA

MSHAMBULIAJI hatari wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Kipre Tchetche, yupo fiti asilimia 100 kuivaa Simba  kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) utakaofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam keshokutwa Jumapili. Mchezo huo ni muhimu kwa Azam FC inayodhaminiwa na Benki ya NMB katika kuendeleza mbio za kuwania ubingwa wa ligi hiyo walioupoteza msimu uliopita baada ya kuchukuliwa na Yanga. Tchetche...

YANGA YAENDELEA KUJIWEKA FITI

KLABU ya Dar Young Africans imeendelea na mazoezi huko mwanza katika viwanja vya DIT wakijiandaa na mchezo wao dhidi ya Toto Africans ambao utachezwa siku ya Jumamosi April 30, Yanga ambayo inashika nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa ligi, wanaelekea katika mchezo huo huku wakijua wazi msimamo wa ligi bado hauwahakikishii ushindi wa moja kwa moja wa ligi ukizingatia wamebakiwa na mechi 5 ambazo zote watacheza ugenini na hivyo kuhitaji ushindi...

SIMBA WAREJEA DAR TAYARI KWA KUIVAA AZAM FC

TIMU ya Simba Sports Club imewasili jijini Dar wakitokea visiwani Zanzibar ambako walikwenda kujiandaa na mchezo wao dhidi ya Azam FC. Simba inayoshika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi inahitaji ushindi katika mchezo huo ili kujiweka katika nafasi mzuri zaidi ya kushindania taji hilo la ligi msimu huu. Siku za hivi karibuni kumekuwa na kutokuelewana kwa baadhi ya wachezaji wa Klabu hiyo na kocha Mayanja kwa kile kinachoelezwa kuwa ni utovu...

Thursday, April 28, 2016

Arsenal Wakiwapata Wachezaji Hawa 3 Wa Seria A, Watamaliza Tatizo La Ushambuliaji

Arsenal wanahitaji kuboresh kikosi chao katika eneo lao la ushambuliaji, ambalo linaonekana kutokuwa imara kulikochangiwa pia na kuondoka kwa Mshambuliaji Robin Van Persie aliekajiunga na mahasimu wao Man United. Ufungaji wa magoli katika kikosi hicho umekuwa si wa uhakika sana, safu hiyo ikiongozwa na Olivier Giroud na Danny Welbeck wanaofanya vizuri lakini si kwa kiwango kile cha Mholanzi Van Persie. Kupata magoli hasa katika mechi za nyumbani...

Dennis Kitambi Aeleza Siri Ya Ushindi Wao Dhidi Ya Majimaji

KOCHA Msaidizi wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Dennis Kitambi, amesema kuwa maelekezo waliyowapa wachezaji wao ya kuongeza hali ya kupambana mchezoni kabla ya kuanza kipindi cha pili ndio yamepelekea kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 jana jioni dhidi ya Majimaji ya Songea. Kitambi amesema pia mabadiliko waliyofanya ya kumwingiza mshambuliaji Ame Ally kipindi cha pili na kumpumzisha Didier Kavumbagu, nayo yamechangia kuondoka...

Mamadou Sakho Afungiwa Kucheza Mpira

Beki wa Liverpool amekataa kuchukuliwa vipimo kwa mara ya pili baada ya majibu ya vipimo vya kwanza kuonyesha alikuwa anatumia dawa za kupunguza unene ambazo haziruhusiwi kwa wanamichezo. Kukataa huko kumelifanya shirikisho la Mpira barani ulaya UEFA kumfungia mchezaji huyo kwa muda wa siku 30. UEFA wamesema katika tovuti yao kuwa “hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya Mchezaji wa Liverpool Mamadou Sakho kufuatia vipimo vilivyofanyika katika...

Guardiola Aendeleza Rekodi Mbaya Mechi Za Ugenini

KOCHA wa Bayern Muchen Pep Guardiola jana ameshuhudia vijana wake wakishindwa kutamba mbele ya Atletico Madrid iliyo chini ya Diego Simeone. Mechi hiyo ya kwanza ya Nusu fainali Klabu bingwa Ulaya ilizikutanisha Atletico na Bayern katika uwanja wa Vicente Calderon Nchini Hispania. Hii inakuwa ni mechi ya 8 mfululizo Guardiola kushindwa kupata ushindi Ugenini.  Bayern ilikubali kichapo cha goli 1 - 0 kutoka kwa Atletico goli lililofungwa...

Wednesday, April 27, 2016

Huyu Ndiye Afisa Habari Mpya TFF

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemteua Alfred Lucas kuwa Afisa Habari na Mawasiliano mpya wa shirikisho kuanzaia leo Aprili 27, 2016. Alfred anachukua nafasi ya Baraka Kizuguto aliyehamishiwa katika Kurugenzi ya Mashindano kuwa Afisa Mashindano na Meneja wa Mifumo pepe ya Usajili (TMS). Alfred ana uzoefu kutoka vyombo mbalimbali alivyovitumikia kama mwandishi wa habari na mhariri. Kadhalika Alfred kitaaluma amesomea uandishi wa...

Yanga Yatinga Fainali Kombe La Shirikisho

Coastal Union imepoteza mechi ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Yanga baada ya washabiki wake kuwa chanzo cha Mwamuzi kuvunja mchezo huo uliofanyika Aprili 24, 2016 kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga. Uamuzi huo umefanywa na Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana leo (Aprili 27, 2016) jijini Dar es Salaam kwa kuzingatia Kanuni ya 28(2) ya Kombe la Shirikisho. Wakati mechi hiyo inavunjwa,...

Tuesday, April 26, 2016

Liverpool Na Dortmund Vitani Kuwania Saini Ya Gotze

Uongozi wa klabu ya Liverpool unaamini uwepo wa Jurgen Klopp klabuni hapo huenda ukaamua hatima ya Mario Gotze Msimu ujao. Gotze anaeonekana kuto kupata nafasi kwa sasa katika klabu ya Bayern anawindwa huenda akaondoka klabuni hapo mwishoni mwa msimu huu. Liverpool na Borussia Dortmund watapambana katika kuinasa saini ya mchezaji huyo.p. Liverpool wanaonekana kumhitaji mchezaji huyo ambae amewahi kutwaa kombe la dunia akiwa na Timu yake ya...

TAIFA STARS KUCHEZA NA HARAMBEE STARS

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager, inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa na timu ya Taifa Kenya (Harambee Stars) Mei 29, 2016 jijini Nairobi. Mchezo huo wa kirafiki utachezwa jijini Nairobi Mei, 29 mwaka huu, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kwa timu zote mbili kujaindaa na michezo ya kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa Afrika mapema mwezi Juni, 2016. TFF kwa kushirkiana...

West Bromwich Yazima Ndoto Za Ubingwa Spurs, Leicester Pointi Tatu Zinatosha Kutangazwa Mabingwa

West Bromwich Albion imezima ndoto za Spurs baada kuwalazimisha sare ya goli 1 - 1. Spurs walikuwa wakwanza kupata goli kipindi cha kwanza cha mchezo dakika ya 33, goli la kujifunga la Dawson. Hadi timu zinaenda mapumziko Tottenhama walikuwa mbele kwa goli 1 - 0. West Bromwich hawakukata tamaa wakaendelea kupambana na hatimaye dakika ya 73 Dawson yule yule ambae alijifunga goli dakika ya 33 alirekebisha makosa yake na kuifungia timu yake goli...

Farid Mussa Aanza Majaribio La Liga

WINGA machachari wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Farid Mussa, ameanza majaribio rasmi nchini Hispania akiwa na kikosi cha timu ya CD Tenerife inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza nchini humo. Farid, 20, aliyefika juzi nchini humo akitokea Tunisia, Azam FC ilipokwenda kucheza na Esperance ya huko kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika, ambapo usiku wa kuamkia leo alitarajiwa kuwa miongoni mwa wachezaji wa Tenerife watakaocheza...

Monday, April 25, 2016

Mambo 5 Ya Ajabu Yaliyosababisha Mechi Kusimama

Mpira wa miguu una mambo mengi tena mara nyingine unaweza kushangazwa zaidi na mambo ya ajabu yanayotokea viwanjani na kulazimika mechi kusimama kwa muda. Hutokea wachezaji wakiwa wanapambana kuzitafutia ushindi timu zao jambo lisilotegemewa kutokea na kuwaacha wachezaji wameduwaa.  Leo nimekuandalia List ya mambo tano yasiyo ya kawaida yaliyosababisha mechi kusimama kwa muda. 5. Ndege Zisizo na Rubani (Drone) Mwezi  wa kumi...